Tuesday, May 3, 2011

Mei mosi Waziri asherehekea kwa kunywa kikombe

Na Thompson Mpanji,Chunya

Katika kusherehekea siku kuu ya wafanyakazi  mei mosi ambayo kitaifa ilifanyika mjini Morogoro,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri  ya muungano wa Tanzania,Jakaya Kikwete,huko wilayani Chunya  kuna  taarifa ya Waziri mmoja kuhitimisha  shamra shamra za sherehe hizo kwa kupata kikombe kutoka kwa mlemavu wa macho.

Akiongea na mwanablog hii Mkazi wa Kijiji cha Mbuyuni,Bw.Nico Haule amesema Naibu Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi,Mh.Philipo Mulugo jana alikuwa miongoni mwa wananchi waliokwenda kupata tiba ya  kikombe kutoka kwa  mpiga kura wake Mlemavu wa macho,Bw.Simon Mahela aliyedai  kuoteshwa na babu yake marehemu kutibu magonjwa yote sugu ikiwemo na ukimwi kwa muda wa siku 43.

Bw.Haule ambaye pia ni mdau wa masuala ya habari,amesema Bw.Mulugo ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Songwe alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za mei mosi ambazo zilifanyika Chang’ombe,Kata ya Mbuyuni,wilayani Chunya ambapo baada ya kuhitimisha sherehe hizo kwa kutoa msaada wa Sh.200,000  ili kusaidia shughuli za mei mosi ziweze kuendelea yeye na makatibu wake wa jimbo walikwenda kushuhudia  tiba hiyo na hatimaye kupata  kikombe cha tiba na hivyo kukonga nyoyo za wapiga wake  na kumuona ni mwenzao.

Mlemavu huyo wa macho anatoa tiba hiyo  kwa masharti ya matamio ya siku 43 bila kunywa pombe wala kufanya tendo lolote la ndoa amekuwa akitoa huduma kwa familia nzima kuchangia sh.500 ambapo siku ya Ijumaa watoto na wanafunzi wanakunywa kikombe bure.

Hata hivyo Bw.Haule amesema  viongozi kadhaa wa Wilaya ya Chunya akiwemo Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw.Deodatus Kinawiro ameshafika kupata tiba ya mlemavu huyo wakati alipokuwa katika ziara za kikazi.

Mwisho.